• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

Yaliyojiri ziara ya kikazi ya waziri wa Kilimo, wilayani Nyasa

Posted on: September 20th, 2024

BASHE APIGA MARUFUKU KANGOMBA  

WAZIRI wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe amepiga marufuku wafanyabiashara wanaonunua kahawa kwa njia ya Kangomba na kuagiza wakamatwe huku akisisitiza kuwa uwekezaji mkubwa unaofanywa katika zao hilo umelenga kuteka soko la kahawa ya Tanzania kimataifa.

Amesisitiza kuwa serikali kwa sasa inawekeza katika kahawa kwa kugawa miche na mbolea ya ruzuku hivyo,anatarajia kupigwa vita na wafanyabiashara kutokana na kukemea kangomba lakini hatarudi nyuma kwa maslahi ya zao hilo.


Waziri Bashe amesema hayo katika muendelezo wa ziara yake Mkoani Ruvuma mara baada ya kutembelea mashamba, viwanda vya kuchakata kahawa na skimu za umwagiliaji wilayani Mbinga na Nyasa.


“Najua haya maamuzi yatakuwa na maumivu na yatakuwa na kelele, mimi kelele nimezoea, kamateni wanaonunu kahawa kwa kangomba,”amesema.


Amesema, anatarajia vita kubwa dhidi ya wafanyabiashara wanaonunua kahawa kwa njia ya Kangomba na hatarudi nyuma.


“Tutegemee kelele nyingi kutoka kwa wafanyabiashara lakini sipo tayari kuona kangomba katika kahawa.Kelele zitakuwa nyingi watapitishia kwa wakulima tujiandae lakini nasema ili kufikia soko la kimataifa hatuwezi kuvumilia ununuzi usiofaa,”amesema.


Amesisitiza kuwa, hatua ya serikali kuwekeza katika zao hilo, imelenga kuijengea ubora kahawa ya Tanzania kimataifa na kunufaisha wakulima.


“Tunatoa mbolea na miche kwa ruzuku na kuwezesha kilimo hiki kuhimili ushindani dhidi ya kahawa za nchi nyingine,”amesema.


Akiwa katika miradi ya umwagiliaji inayotekelezwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Waziri Bashe amesema“Nimejionea kiwango cha umasikini wa watu wetu hapo mambo tumeanza kuyafanyia kazi.Tunamshukuru sana Rais Dk. Samia Suluhu Hasan kwa kutupatia fedha mwaka huu, nimemwambia Mbunge Injinia Stella Manyanya, tutafanyia kazi changamoto za watu wetu.


“Tumeshatangaza na tumeshapata mkandarasi kwa skimu zenye hekta 8395 tutajenga barabara za ndani ya shamba, madaraja na vigawa maji ndani ya shamba na usanifu umeshakamilika na mkandarasi amepatikana”,amesema Waziri Bashe


Pia Waziri Bashe ameitaka,kufanya usanifu na kuziingiza barabara za Lipingo katika mpango wa utekeleza wa mradi huo wa Umwagiliaji


“Nimegiza Tume ifanye usanifu, waingize kwenye mradi barabara zote mbili hapa Tume inatekelez miradi ya zaidi ya Bilioni 25 kwa Wilaya ya Nyasa pekee haishindwi kujenga hizo barabara zote,”amesema.


Aidha amesisitiza haja ya Skimu zilizopo katika Halmashauri ya Nyasa na idadi ya skimu zitakazo anza kufanyiwa utekelezaji kwa haraka.


“Halmashauri ya nyasa kuna skimu nane na kwa kuanzia tutaanza kuzijenga skimu mbili kuanzia mwaka huu wa fedha na ndani ya miaka 2 zote hizo zitakuwa zimejengwa.Muwape ushirikiano wataalamu wanaotekeleza miradi”


“Pia Tume mfanye ujenzi wa ghala katika eneo la mradi na mashine ya kukoboa mpunga ili wananchi waweze kuuza mchele badala ya Mpunga,”amesema.


Ameongeza kuwa Wizara ina mpango wa kuanza kuzalisha wa mbegu karibu na eneo la mradi wa Lundo katika kata ya Lipingo na kuanzisha vituo vya zana za kilimo na kujenga kituo cha mbolea.


Naye, Mbunge wa Jimbo la Nyasa Injinia Manyanya, amesema Wilaya hiyo inahitaji kukua kiuchumi na tegemeo kubwa ni kilimo cha mpunga hivyo wanatarajia miradi ya umwagiliaji iwe chachu ya uzalishaji.

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Jela maisha Kwa Ubakaji

    May 27, 2025
  • Msigwa aipongeza Tamisemi kikao maafisa habari

    May 24, 2025
  • SERIKALI ilivyodhamiria kuboresha Barabara na madaraja

    May 23, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wapitia miradi 76 mkoa wa Ruvuma

    May 17, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.