• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

WAZIRI TAMISEMI ATANGAZA AJIRA ZA WALIMU NA KADA ZA AFYA.

Posted on: May 9th, 2021

OFISI ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imepata kibali cha ajira za walimu wa shule ya msingi na sekondari 6,949 na kada mbalimbali za afya 2,726 watakaoajiriwa chini ya Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.

Maombi ya ajira hizo yataombwa kwa njia ya mtandao kuanzia Mei 9 hadi 23, mwaka huu kupitia kiunganishi cha ajira.tamisemi.go.tz.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Ummy Mwalimu, amesema ajira hizo zitajaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliokoma utumishi kutokana na sababu mbalimbali.

“Serikali imetoa kibali, maana mara baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kueleza kwamba atatoa ajira 6000 kwa walimu tulikuwa tunapata msukumo mkubwa kutoka kwa wananchi wakihoji kwanini TAMISEMI hatutangazi, taratibu za serikali lazima tupate kibali Menejimenti ya Utumishi wa umma,”amesema.

Hata hivyo, amesema serikali imetoa fursa kwa waombaji ambao ni walemavu kutuma maombi yao kwa nakala ngumu na yaeleze aina ya ulemavu wao na picha zao na kutumwa kwa anuani ya Katibu Mkuu TAMISEMI na Ofisi ya Waziri Mkuu ili aione Mkurugenzi wa kitengo cha watu wenye ulemavu.

Akitaja sifa za waombaji wa ualimu, Waziri Ummy amesema kwa shule ya msingi wanatakiwa walimu wenye daraja la IIIA kuwa astashahada ya elimu ya msingi, elimu ya michezo, elimu ya awali na elimu maalum.

“Mwalimu wa daraja la IIIB anatakiwa kuwa mhitimu wa stashahada ya ualimu wa elimu ya awali, msingi, elimu maalum na Mwalimu wa daraja la IIIC, mhitimu wa shahada ya ualimu masomo ya lugha ya kiingereza, historia na jiografia,”amesema.

Kadhalika, amesema kwa shule za sekondari wapo kwenye makundi manne ambapo anatakiwa mwalimu wa daraja IIIB ambaye amehitimu stashahada ya ualimu wa masomo ya Fizikia, Hesabu, Baiolojia na Kemia.

“Pia mwalimu wa daraja IIIC ambaye amehitimu ualimu aliyesomea elimu maalum kwa masomo hayo na shahada ya ualimu wa masomo hayo, pia awe amehitimu stashahada ya uzamili katika elimu lazima awe mwenye shahada ya kwanza yenye masomo tajwa,”amesema.

Pia amesema kwa waombaji wa ajira hizo ambao wamesomea elimu ya sekondari nje ya nchi wanatakiwa kupata namba ya ulinganifu wa matokeo inayoanzia na herufi EQ…kutoka Baraza la Mitihani la Tanznaia ili kuingia kwenye mfumo wa maombi ya ajira.

“Pia wanatakiwa kupata ithibati ya masomo yao kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), ili vyeti vyao vitambulike na kupata uhalali wa kutumika nchini,”amesema.

Pamoja na hayo, Ummy amesema kada za afya ambazo serikali itaajiri ni daktari daraja la II, daktari wa meno daraja la II, tabibu daraja la II, tabibu msaidizi, tabibu wa meno daraja la II, tabibu meno msaidizi, mfamasia daraja la II.

Nyingine ni mteknolojia wa dawa daraja la II, mteknolojia msaidizi wa dawa, mteknolojia wa maabara daraja II, mteknolojia msaidizi maabara, mteknolojia mionzi daraja la II, mteknolojia msaidizi wa mionzi, mteknolojia wa macho daraja la II.

Kadhalika, alisema itaajiri Ofisa Muuguzi daraja la II, Ofisa muuguzi msaidizi daraja la II, Muuguzi daraja la II, mtoa tiba kwa vitendo daraja la II, Ofisa afya mazingira daraja la II, Ofisa afya mazingira msaidizi daraja la II, Msaidizi wa afya, Katibu wa afya daraja la II, Ofisa ustawi wa jamii daraja la II na Ofisa lishe daraja la II.


Amesema ajira zitatolewa kwa haki na hataruhusu kuwepo na aina yeyote ya ushawishi  na kusisitiza watazingatia wale waliomba kwa maelekezo yaliyotolewa.

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • RAIS SAMIA AMWAGA MAMILIONI YA EDHA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA NYASA DC

    June 28, 2025
  • RAIS SAMIA AMWAGA MAMILIONI YA EDHA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA NYASA DC

    June 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA JAMII

    June 26, 2025
  • KICHEKO CHATAWALA TAFRIJA YA KUWAAGA MADIWANI

    June 19, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.