• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

WANAUME WAOGA KUPIMA AFYA ZAO WAHAMASISHWA.

Posted on: October 25th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabela Chilumba amewataka wanaume kuwa majasiri wa kupima afya zao badala ya kutegemea majibu ya wenza wao ambao hupima virusi vya UKIMWI kwa lazima wakiwa wajawazito.

Ameyasema hayo wakati akizindua kampeni ya pima jitambue ishi kwa furaha Kiwilaya iliyofanyika jana katika Kijiji cha Litumbakuhamba kata ya Linga Wilayani hapa yenye lengo la kuwahamasisha wanaume kupima afya zao na kujitambua kama wameambukizwa virusi vya UKIMWI ili waweze kuanza kutumia vidonge vya kufubaza virusi vya UKIMWI na ambao hawajaathirika kuchukua tahadhari.

Mkuu wa Wilaya alifafanua kuwa wanaume wengi ni waoga kwenda kupima na kujua afya zao na wanategemea majibu ya wenza wao wakishapima huwauliza vipi majibu mke wake akisema sina maambukizi na mwanaume naye husema hana maambukizi lakini kama mke wake akiwa na maambukizi naye huomba vidonge na kuanza kumeza na huona aibu kwenda kuchukua dawa na hujikuta dozi ya mkewe hugawana wote hali inayoweza kuleta usumbufu miongoni mwao kwa kuwa dawa hizo hutolewa kwa kdozi ya kila mgonjwa.

Aliongeza kusema kuwa lengo la kampeni hiyo ni kuhakikisha kila mwanamke na mwanaume wanapima virusi vya UKIMWI na kujitambua ili waweze kuishi wakiwa na uhakika wa afya zao na wachukue hatua ya kuanza dawa mara baada ya kugundulika wameambukizwa na kwa wale ambao hawajambukizwa wachukue taadhari ya kutunza afya zao.

“Katika maisha tunaamini kuwa wanaume ni majasiri si ndio jamani,lakini kwa siku ya leo napenda kuwaambia kuwa hakuna watu waoga kama hawa wanaume katika kupima virusi vya UKIMWI.Wengi wao wanategemea majibu ya wake zao ili waweze kujua afya zao,lakini kitendo hicho sio kweli kwa kuwa kila mtu anakuwa na afya yake na mwenendo wake.kuna wakati mke ni anakuwa ameathirika na mwanaume ni mzima na wakati mwingine mume kaathirika na mke anakuwa hana maambukizi hivyo ni wajibu wa kila mtu kujua afya yake ili aweze kuishi kwa furaha”.

Wananchi waliokuwepo walifurahia kuhamasishwa huko na wakasema wataendelea kupima afya zao ili waweze kujitambua na kutoa ahadi kwa mkuu huyo watakuwa wanaenda kupima na kujua hali zao za afya.

Awali akitoa taarifa ya upimaji wa virusi vya UKIMWI wilayani Nyasa Kaimu Mganga Mkuu Dkt Aron Hyera alisema mwamko wa upimaji wa virusi vya UKIMWI unaendelea vizuri watu wengi wanahamasika kupima na kwa mwaka huu jumla ya wanaume 79599 sawa na asilimia 56 walipima na kujua afya zao na akinamama 32139 sawa na asilimia 44 walipima afya zao katika Wilaya ya Nyasa.

Katika hatua nyingine Wananchi hao wa kijiji cha Litumbakuhamba waliomba zahanati yao iboreshwe iweze kutoa huduma ya dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI kwa kuwa kwa sasa wanapata shida ya kwenda kupata huduma hiyo katika kata ya lituhi ambako ni mbali kutoka katika kijiji Hicho.

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • RAIS SAMIA AMWAGA MAMILIONI YA EDHA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA NYASA DC

    June 28, 2025
  • RAIS SAMIA AMWAGA MAMILIONI YA EDHA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA NYASA DC

    June 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA JAMII

    June 26, 2025
  • KICHEKO CHATAWALA TAFRIJA YA KUWAAGA MADIWANI

    June 19, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.