• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

Wananchi watakiwa kuacha Mila zinazosababiasha maambukizi ya HIV

Posted on: December 1st, 2024

WANANCHI WATAKIWA KUACHA MILA ZINAZOCHOCHEA MAAMBUKIZI YA VVU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, amewataka wananchi wa Tanzania kuzingatia Elimu inayotolewa kupitia kampeni mbalimbali ili kuachana na mila zinazoweza kuwa vichocheo vya maambukizi ya VVU.

Ametoa rai hiyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo kitaifa imefanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma.

"Ninaendelea kutoa rai kwa watanzania kuzingatia maudhui ya Elimu inayotolewa kupitia kampeni mbalimbali, kuachana na mila zinazoweza kuwa vichocheo vya maambukizi na kuendelea kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI," alisema Mhe. Dkt. Mpango.

Ameongeza kuwa kundi la vijana hasa wa kike wapo kwenye hatari zaidi ya kupata VVU, hivyo ameiagiza Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) kushirikiana na wadau na jamii kwa ujumla kuweka mkazo katika kudhibiti mazingira yanayochochea maambukizi.

Kupitia maadhimisho hayo ametoa wito kwa vijana kujitambua, kujithamini na kutunza maisha yao kwa kujikinga dhidi ya maambukizi mapya ya VVU, na ambao wanaishi na maambukizi kuendelea kutumia dawa za kufubaza makali ya virusi kwa usahihi na kuimarisha afya zao.

Kwa upande mwingine Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ya mwaka huu ambayo inasema Chagua Njia Sahihi, Tokomeza UKIMWI inakumbusha umuhimu wa kuwa na mikakati na mbinu bora za kuendelea kushirikisha jamii ili kufikia malengo ya kuwa na Tanzania isiyo na maambukizi ya VVU ifikapo mwaka 2030.

Hata hivyo amesema kuwa maadhimisho hayo mwaka huu yanatoa msisitizo kwa vijana kuendesha mijadala na kuwa na matukio mbalimbali ili kuwawezesha kupata Elimu kwa pamoja kuhusiana na masuala ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Naye Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, amesisitiza kuwa Wizara ya Afya itaendelea kuongeza jitihada kuhakikisha inafanya mapitio ya kisera, mikakati na miongozo ya kutoa huduma bora kwa jamii katika afua zote za mwitikio dhidi ya VVU na UKIMWI.

Amesisitiza kwamba UKIMWI bado upo, hivyo Taifa lina kila sababu ya kuendelea kuzuia maambukizi mapya na kuhakikisha walio na maambukizi wanafubaza VVU.

Siku ya UKIMWI Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 1 Desemba ambayo inalenga kueneza ufahamu kuhusu UKIMWI, kuwakumbuka waliopoteza maisha kutokana na UKIMWI,  kuhamasisha hatua za kuzuia maambukizi mapya, na kupambana na unyanyapaa unaohusiana na VVU au UKIMWI.

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Jela maisha Kwa Ubakaji

    May 27, 2025
  • Msigwa aipongeza Tamisemi kikao maafisa habari

    May 24, 2025
  • SERIKALI ilivyodhamiria kuboresha Barabara na madaraja

    May 23, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wapitia miradi 76 mkoa wa Ruvuma

    May 17, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.