• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

WAFANYAKAZI RUVUMA WALIA NA MISHAHARA MIDOGO

Posted on: May 2nd, 2021

WAFANYAKAZI mkoani Ruvuma wamelalamikia mishahara yao kuwa bado ni midogo ukilinganisha na hali halisi ya maisha ya wafanyakazi.

Akisoma risala ya wafanyakazi wa Mkoa wa Ruvuma katika sherehe ya Mei Mosi iliyofanyika kimkoa mjini Mbambabay wilayani Nyasa,Katibu wa TUGHE Mkoa wa Ruvuma Ismail Mudathir amesema katika sekta ya umma na binafsi mishahara haikidhi mahitaji ukilinganisha na kupanda kwa gharama za maisha.

“Tunaiomba serikali kupitia Mei Mosi hii,kwa itutazame jicho la kipekee kabisa iongeze mishahara na kuboresha maslahi kwa wafanyakazi kwa sababu ni muda mrefu sana mishahara haijaongezwa’’,alisisitiza Katibu wa TUGHE.Amesema watumishi wa Mkoa wa Ruvuma,wanakabiliwa na changamoto za kiutumishi zikiwemo baadhi ya waajiri kutowatendea haki baadhi ya watumishi hali ambayo ina punguza molali kwa wafanyakazi.

Amezitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni kutolipwa madeni ya uhamisho wa watumishi,baadhi ya watumishi kutopandishwa madaraja kwa wakati na baadhi ya waajiri kutolipa nauli za watumishi na mizigo yao wanapostaafu.

Hata hivyo licha ya changamoto hizo Katibu huyo wa TUGHE kwa niaba ya watumishi mkoani Ruvuma amesema,wafanyakazi wanaahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa maslahi mapana ya nchi ya Tanzania.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba ametoa rai kwa watumishi kuwa na subira kwa sababu serikali ya Awamu ya sita imedhamiria kuboresha maslahi ya watumishi.

“Serikali mwezi huu imeanza kutoa barua za kuwapandisha madaraja watumishi wa umma wanaostahili katika nchi nzima na katika Halmashauri za wilaya baadhi ya watumishi wameanza kupata barua za kupandishwa madaraja kupitia maafisa utumishi’’,alisema Chilumba.

Hata hivyo amewaagiza waajiri kuhakikisha wanawalipa mafao na haki zao zote watumishi wanaostaafu na kuwaagiza waajiri kwenye Halmashauri na Taasisi zote za serikali kuacha kuchelewesha fedha za malipo ya likizo kwa watumishi wanaokwenda likizo.

Mei Mosi ni siku ya wafanyakazi wote duniani inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo Mei Mosi,kauli mbiu ya mwaka huu ni maslahi bora,mishahara juu,kazi iendelee.

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Jela maisha Kwa Ubakaji

    May 27, 2025
  • Msigwa aipongeza Tamisemi kikao maafisa habari

    May 24, 2025
  • SERIKALI ilivyodhamiria kuboresha Barabara na madaraja

    May 23, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wapitia miradi 76 mkoa wa Ruvuma

    May 17, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.