• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

Visiwa vitatu vinavyofungua Utalii Nyasa

Posted on: April 22nd, 2025

VISIWA VITATU VINAVYOFUNGUA UTALII NYASA

Katika pembe ya kusini mwa Tanzania,Ziwa Nyasa Wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma kuna hazina ya asili ambayo bado haijagunduliwa na wengi .


Visiwa vitatu vya Mbambabay, Lundo na Puulu,hivi si visiwa vya kawaida; ni visiwa vyenye hadithi, historia na mandhari ya kuvutia kiasi cha kuibua hisia na hamu ya kutaka kufahamu zaidi.


Mbambabay: Kisiwa cha Mapango na Samaki wa Mapambo


Kisiwa cha Mbambabay, kinachotajwa kuwa moja ya vivutio vya utalii wa kipekee, kimejaa mapango yanayotumika na wavuvi kama hifadhi salama wakati wa dhoruba kali.


Ni mahali pa asili ambapo mazingira yanazungumza ,hewa safi, sauti za ndege, na mwonekano wa samaki wa mapambo wanaoangaza chini ya maji safi ya Ziwa Nyasa.


Kwa wapenzi wa mazingira ya kuvutia na utulivu, kisiwa cha Mbambabay ni patanisho  na sehemu asili  inayovutia wengi.


Lundo: Historia Yenye Machungu na Mafundisho


Kisiwa cha Lundo kinabeba simulizi ya binadamu na jamii ,historia ya wagonjwa wa ukoma waliotengwa na kupelekwa kuishi kisiwani humo wakati wa utawala wa wajerumani


Makaburi ya waliopoteza maisha yao kutokana na ugonjwa huo bado yapo, yakielezea namna jamii ya wakati huo ilivyokabiliana na hofu ya maradhi.


Waliopoteza maisha walizikwa kwa kufunikwa na tope, imani ikisema hilo lingesaidia kutokomeza ugonjwa wa ukoma.


Lundo si tu kivutio cha kiasili, bali pia mahali pa kutafakari kuhusu historia, utu na maendeleo ya kijamii.


Puulu: Makazi ya Ndege wa Ajabu


Kisiwa cha Puulu, kilichopo Kata ya Liuli, ni mahali panapopaswa kutembelewa na kila mpenda maajabu ya asili.


Kisiwa hiki Kina mazalia ya samaki wa aina nyingi, wakiwemo wale wa mapambo. Lakini kivutio cha kipekee zaidi ni ndege maarufu duniani ajulikanaye kama ngwazi, anayejulikana kwa ustadi wake wa kipekee wa kuvua samaki kutoka majini.


Visiwa hivi ni hazina ambayo inahitaji kuangaziwa zaidi, kutangazwa kitaifa na kimataifa, na kuwekewa miundombinu rafiki ili kuwavutia watalii wa ndani na wa kimataifa.


Wilaya ya Nyasa, kupitia vivutio hivi, inaweza kuwa kitovu kipya cha utalii endelevu kusini mwa Tanzania

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Karibu Mwenge wa Uhuru Wilayani Nyasa

    May 11, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume huru ya Uchaguzi Tanzania akagua vituo vya kujiandikisha Nyasa.

    May 04, 2025
  • Dc Nyasa awataka madiwani na watendaji kubuni vyanzo vipya vya mapato

    April 30, 2025
  • DC Nyasa azindua Kituo kipya cha Mafuta

    April 26, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.