• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi Bora ya Ardhi (NLUPC) kupanga vijiji 14 Nyasa)

Posted on: October 13th, 2024


Kaimu Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Ruvuma Bw. Shadrack Peter Kansimba amepokea na kuwakaribisha wataalamu wa kutoka Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) wanaotarajiwa kukita kambi katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwa ajili ya kuwezesha uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 14 vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.

Akizungumza mbele ya wataalamu hao waliofika Ofisi za Ardhi Mkoani humo kwa ajili ya kutambulisha zoezi la uandaaji mipango ya matumizi ya ardhi Wilayani Nyasa, Kaimu Kamishna Kansimba ameishukuru Serikali kupitia Tume kwa kuleta zoezi hilo Mkoani Ruvuma ambapo anaamini litatua changamoto za migogoro na kuahidi kutoa ushirikiano wakati wote wa utekelezaji wa zoezi hilo.

“Mkoa wa Ruvuma ni moja ya Mikoa inayokumbana na changamoto nyingi za migogoro baina ya watumiaji mbalimbali wa ardhi, hivyo kuja kwa zoezi hili kutasaidia kuondoa migogoro na kuongeza idadi ya Vijiji vitakavyokua vimeandaliwa mpango wa matumizi ya ardhi” alisema Bw. Kansimba

Bw. Kansimba aliendelea kusisitiza kuwa, Ofisi ya Ardhi Mkoa itakuwa tayari kutoa wataalamu pindi watakapohitajika ili kushirikiana na wataalamu kutoka Tume na Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa endapo itahitajika kuongeza nguvu itakayopelekea kukamilisha kazi kwa muda uliopangwa.

Wakati huo huo, timu hiyo ya wataalamu kutoka Tume imewasili Wilayani Nyasa, na kuanza moja kwa moja hatua za awali za uandaaji matumizi ya ardhi ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo Timu Shirikishi ya Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi ya Wilaya (Participatory Land Use Management Team – PLUM).

Katika awamu ya kwanza Vijiji vitakavyoandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi ni Kwambe, Tumbi, Ng’ombo, Chimate, Ng’indo, Ndonga na Kiagara. Aidha, awamu ya pili itakuwa na vijiji vya Mitomini, Mkalawa, Mipotopoto, Kwangwai, Uhuru, Mkili na Nandonga.

Uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi ya Vijiji katika Halmashauri hiyo ni utekelezaji wa Mradi wa Upangaji Matumizi ya Ardhi uliojikita kwenye Wilaya na Vijiji vinavyopitiwa na Miradi mikubwa ya Kimkakati, Vijiji vyenye Migogoro ya matumizi ya ardhi pamoja na Vijiji vilivyopo kwenye Wilaya za mipakani.

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Jela maisha Kwa Ubakaji

    May 27, 2025
  • Msigwa aipongeza Tamisemi kikao maafisa habari

    May 24, 2025
  • SERIKALI ilivyodhamiria kuboresha Barabara na madaraja

    May 23, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wapitia miradi 76 mkoa wa Ruvuma

    May 17, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.