• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

RC IBUGE, AZINDUA MAADHIMISHO YA SIKU YA MBOLEA DUNIANI

Posted on: October 12th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amezindua maadhimisho ya siku ya mbolea duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Kabla ya kuzindua maonesho hayo RC Ibuge alikagua vibanda 41 vya washiriki wa maonesho ambayo yanafanyika kuanzia Oktoba 11 na kilele chake ni Oktoba 13.

Akizungumza na wananchi kwenye uzinduzi huo Mkuu  wa Mkoa wa Ruvuma,amesema Mkoa una chakula cha kutosha kwa muda mrefu ambapo katika msimu wa mwaka 2020/2021,Mkoa wa Ruvuma umezalisha tani 1,384,705 za mazao yote ya chakula na kuwa na ziada ya tani 894,960.

‘’Kwa zao la mahindi pekee uzalishaji ni tani 816,242 hivyo kuwa na ziada ya jumla ya tani 326,497 za mahindi’’,alisisitiza RC Ibuge.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,amesema uzalishaji huo unaambatana na matumizi ya pembejeo bora ikiwemo mbolea .

Ameyataja mahitaji ya mbolea katika Mkoa wa Ruvuma kuwa ni jumla ya tani 50,521 kwa msimu wa  kilimo wa mwaka 2020/2021 ambapo mbolea zilizoingia na kutumika ni tani 43,000 na kwamba katika msimu wa kilimo wa mwaka 2021/2022 Mkoa unatarajia kutumia mbolea tani 50,521 za aina zote za mbolea.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Dkt.Stephano Ngailo  ameutaja mkakati mkuu wa serikali ni kuhakikisha kuwa mbolea inapatikana kwa wingi na bei nafuu kwa kuwekeza kwenye ujenzi wa viwanda vya mbolea hapa nchini.

Amesema serikali imeanza ujenzi wa kiwanda cha mbolea mkoani Dodoma ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha mbolea za aina mbalimbali zaidi ya tani laki sita kwa mwaka.

Dkt.Ngailo amesema kiwanda hicho kinatarajia kuanza uzalishaji msimu wa mwaka 2022/2023,  ambacho amesema kitakuwa ni ukombozi mkubwa kwa wakulima hapa nchini wakiwemo wa Mkoa wa Ruvuma ambao wanaongoza kwa kuzalisha mazao ya chakula nchini.

Kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya mbolea duniani ni tumia mbolea bora, kwa tija na kilimo endelevu.

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Jela maisha Kwa Ubakaji

    May 27, 2025
  • Msigwa aipongeza Tamisemi kikao maafisa habari

    May 24, 2025
  • SERIKALI ilivyodhamiria kuboresha Barabara na madaraja

    May 23, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wapitia miradi 76 mkoa wa Ruvuma

    May 17, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.