• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

RAIS SAMIA AISHUKURU BENKI YA MAENDELEO AFRICA KWA UWEZESHAJI KWENYE MIUNDOMBINU

Posted on: September 26th, 2024

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameishukuru na kuipongeza Taasisi ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuwa mdau mkubwa wa sekta ya miundombinu nchini ambapo wamewezesha mkopo wa Shilingi Bilioni 630 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 66) kwa kiwango cha lami na barabara nyingine.

Dkt. Samia ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na wananchi Wilayani Nyasa mara baada ya kufungua barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 16) iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi Bilioni 122.76 Mkoani Ruvuma.

“Nataka niwaambie benki ya AfDB hawajasaidia barabara hii peke yake, ni wadau wetu wa barabara nchi nzima na hivi tunavyozungumza wanatusaidia kujenga barabara ya mzunguko ya njia nne katika mji Mkuu wa Dodoma”, Amekaririwa Dkt. Samia.

Dkt. Samia ameeleza kuwa kukamilika kwa barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 66) kwa kiwango cha lami utasaidia kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa abiria na bidhaa na amewataka wananchi kutumia uwepo wa barabara hiyo kuleta maendeleo katika Wilaya ya Nyasa na Mkoa wa Ruvuma kiujumla.

Aidha, Dkt. Samia ametoa wito kwa watumiaji wa barabara hiyo hususani madereva kuwa waangalifu ili barabara iweze kudumu kwa muda mrefu zaidi.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuendelea kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ambapo wamekamilisha kujenga kwa kiwango cha lami mtandao wa barabara zenye urefu wa kilometa 2,384 ambayo ni sawa na asilimia 20 ya mtandao wote wa barabara unaosimamiwa na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS).

Kadhalika, Bashungwa ameeleza kuwa Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS ipo katika hatua za kutafuta Wakandarasi kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni Daraja la Mkili lenye urefu wa mita 20 pamoja na Daraja la Mitomoni lenye urefu wa mita 80 ambalo litaunganisha Wilaya ya Nyasa na Songea Vijijini.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Patricia Laverley, ameleeza utekelezaji wa mradi huo ni sehemu ya urafiki kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki hiyo na kusema kuwa kukamilika kwa barabara ya Mbinga – Mbamba Bay kutasaidia kupunguza muda wa safari, nauli pamoja na gharama za matengenezo.

Awali akitoa taarifa ya mradi huo, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta ameeleza kuwa Barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 66) imefadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika chini ya mradi wa “Transport Sector Support Programme” (TSSP) na kutekelezwa na Mkandarasi China Henan International Cooperation Group kutoka China na Mhandisi Mshauri kutoka SMEC International Pty kutoka Australia kwa gharama ya Shilingi Bilioni 122.76


Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Karibu Mwenge wa Uhuru Wilayani Nyasa

    May 11, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume huru ya Uchaguzi Tanzania akagua vituo vya kujiandikisha Nyasa.

    May 04, 2025
  • Dc Nyasa awataka madiwani na watendaji kubuni vyanzo vipya vya mapato

    April 30, 2025
  • DC Nyasa azindua Kituo kipya cha Mafuta

    April 26, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.