• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ahamasisha Wawekezaji kuwekeza Nyasa, Sekta ya Utalii

Posted on: July 29th, 2021



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amewataka wawekezaji nchini kuwekeza kwenye vivutio vya utalii vinavyopatikana katika Wilaya ya Nyasa ili kukuza uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi wa eneo hilo.




Amesema hayo leo wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua maeneo ya utalii kwa lengo la kuyaboresha katika ufukwe wa Mpela, kijiji cha Kihagara Wilaya ya Nyasa leo.

“Tutaitangaza Nyasa kuhakikisha kwamba wawekezaji wanakuja Nyasa kuwekeza kwenye fukwe zetu” amesema Mhe. Mary Masanja.

Mhe. Mary Masanja amefafanua kuwa vivutio vya utalii vinavopatikana katika Wilaya ya Nyasa ni vya kipekee.

“Nyasa kuna vivutio vya kipekee kama bustani ya mawe, kuna ziwa Nyasa lenye ufukwe mzuri wenye maji safi, kuna mamba wanaoweza kuwasiliana na binadamu na kuna ngoma za asili zinazohamas” Mhe. Masanja amesema.

Ili kukuza utalii huo, Mhe. Masanja amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kupima maeneo yote ya fukwe na kuyatangaza kwa wawekezaji ili yaanze kuingiza mapato kwa Taifa na kufaidisha wananchi wa maeneo hayo.

Aidha, Mhe. Masanja ameelekeza kuanzishwe matamasha mbalimbali yatakayovutia watalii kutembelea eneo hilo.

“Tutengeneze matamasha ambayo yatavutia wageni kutembelea hapa na tutacheza ngoma zetu za asili ili wageni waone kilichopo hapa na tutaweka viingilio ili wageni wakija waache chochote kitakachowafaidisha wenyeji” Mhe. Masanja amesema

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mhe. Kanali Laban Thomas amesema vivutio vinavyopatikana Nyasa havipatikani sehemu yoyote duniani.

Amemshukuru Mhe. Mary Masanja kwa kuhamasisha na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Wilaya ya Nyasa.

“Tunashukuru kwa kuendelea kuhamasisha na kuelimisha watu kuhusu utalii wa Nyasa kwa sababu watu wengi huwa wanaamini utalii ni wa wanyamapori tu” amefafanua Mhe. Thomas.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mhe. Eng. Stella Manyaya amesema Nyasa iko tayari kwa ajili ya kutangaza vivutio vyake vya utalii.

Pia, Mhe. Manyanya amemshukuru Mhe. Mary Masanja kwa kutumia muda wake kutangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana katika jimbo lake.

Ziara ya kikazi ya Mhe. Mary Masanja Wilayani Nyasa ni mwendelezo wa ziara zake za kikazi za kukagua maeneo yenye vivutio vya utalii na kuangalia namna bora ya kuyaboresha ili yaanze kutumika kuingiza mapato yatokanayo na utalii.

 


 

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Jela maisha Kwa Ubakaji

    May 27, 2025
  • Msigwa aipongeza Tamisemi kikao maafisa habari

    May 24, 2025
  • SERIKALI ilivyodhamiria kuboresha Barabara na madaraja

    May 23, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wapitia miradi 76 mkoa wa Ruvuma

    May 17, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.