• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma azindua soko la mahindi Songea

Posted on: August 16th, 2021


MKOA wa Ruvuma katika kipindi cha mwaka 2020/2021 umezalisha ziada ya mahindi tani 326,497 kati ya tani za mahindi 816,242 zilizozalishwa.

Akizungumza wakati anazindua soko la ununuzi wa zao la mahindi Kanda ya Songea mkoani Ruvuma katika kijiji cha Mgazini Halmashauri ya Songea,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema katika kipindi cha mwaka 2020/2021,wakulima wa mahindi wameweza kulima jumla ya hekta 276,488.

“Uzalishaji huu ni zaidi ya kiwango kilichozalishwa kwa ongezeko la asilimia nne,ukilinganisha na kiwango cha uzalishaji katika msimu wa mwaka 2019/2020 ambapo tani 787,321 pekee zilizalishwa’’,alisisitiza Ibuge.

Brigedia Jenerali Ibuge amesema Mkoa una uwezo wa kuuza ziada hiyo ya mahindi ndani na nje ya nchi ambapo amewapongeza Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA kwa uamuzi wa kununua mahindi ambayo ni sehemu ya ziada.

Amesema katika awamu ya kwanza ya ununuzi kutakuwa na vituo tisa  katika Mkoa wa mzima ambavyo vimepangwa kwa lengo la kumrahisishia mkulima kuweza kununua mahindi yake bila kutumia gharama kubwa.

Hata hivyo amesema kiwango cha kununua tani 32,000 tu za mahindi kwa Mkoa wa Ruvuma ambacho kimewekwa na NFRA ni kidogo ukilinganisha na uzalishaji mkubwa wa mahindi uliofanywa na wakulima msimu huu.

Amesema mgawo huo ni kidogo hivyo ametoa rai kwa Wizara ya Kilimo  kupitia NFRA kuendelea kushirikiana kupanua wigo wa masoko ili wakulima wa Ruvuma waendelee kuzalisha ziada.

Ametoa rai kwa wanunuzi wengine nchini kote  kufika mkoani Ruvuma kuendelea kununua mahindi ili kuipunguza ziada iende kwa wengine nje ya nchi na maeneo mengine yenye uhaba wa chakula ambapo amewaomba kununua kwa bei nzuri ili kuleta tija kwa wakulima na kuwawezesha kulima kwa tija zaidi.

Awali Meneja wa NFRA Kanda ya Songea Ramadhani Nondo  alisema  kwa ujumla NFRA katika msimu wa mwaka 2020/2021,wanatarajia kununua tani za mahindi 165,000 ambapo  Kanda ya Songea imetengewa kununua mahindi tani 32,000 na kwamba kwa awamu ya kwanza zinanunuliwa tani 6,000 za mahindi.

Amesema mahindi yatanunuliwa kwa shilingi 500 kwa kilo katika kituo cha NFRA Ruhuwiko na vituo vingine mahindi yatanunuliwa kwa kilo shilingi 470 na kwamba ununuzi utafanyika kwenye vituo tisa vilivyopangwa ambavyo amevitaja kuwa ni Namtumbo mjini, Namabengo,Mgazini,Magagura,Mpitimbi,Mbinga mjini,Kigonsera na Ofisi za Kanda za NFRA Ruhuwiko.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Odo Mwisho ameiomba serikali iongeze kiwango cha tani za ununuzi  kwa sababu wananchi watauza kiasi kidogo cha mahindi ukilinganisha na uzalishaji,hivyo ameshauri  serikali inunue mahindi kupitia mfuko mkuu wa serikali ili yakauzwe kwenye mahitaji ya chakula ndani na nje ya nchi.

Amesisitiza kuwa wananchi wasipotafutiwe masoko ya uhakika ya mazao yao,wataendelea kupata hasara kwa kuuza kwa bei ndogo hali ambayo itawakatisha tamaa kuendelea kulima zao la mahindi.

Mkoa wa Ruvuma kwa mwaka wa tatu mfululizo umeendelea kushika nafasi ya kwanza kitaifa kwa kuongoza kwa uzalishaji wa mazao ya chakula.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Agosti 16,2021

Announcements

  • Fursa ya kuwekeza kilimo cha Korosho shamba Wilaya ya Nyasa October 24, 2024
  • TANGAZO la kuitwa kwenye Usaili wa waandishi Wasaidizi na waendeshaji Vifaa vya Bayometriki (BVR) December 18, 2024
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • View All

Latest News

  • UTEKELEZAJI KAMPENI YA CHANJO YA MIFUGO YAANZA NYASA

    July 12, 2025
  • MAKUNDI SOGOZI YA WHATSAAP YAPASWA KUJADILI MAENDELEO

    July 12, 2025
  • DC MAGIRI AZINDUA RASMI BODI YA MAJI WILAYA YA NYASA

    July 12, 2025
  • DKT.SAMIA AMWAGA TENA MAMILIONI YA MIRADI NYASA

    July 10, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.