• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Nyasa District Council
Nyasa District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Nyasa District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Organisation Structrure
  • Services
    • Water services
    • Education services
    • Health services
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • primary education
      • secondary education
      • planning,statistics and monitoring
      • Agriculture,Irrigation and Cooperative
      • Community Development, Social Welfare and Youth
      • Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescure
      • Environmental and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Water
      • Land and Natural Resource
      • Health
    • Unity/Sections
      • Information and Communication Technology
      • Legal
      • Internal Auditor
      • Procurement and Supply
    • Full Council
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
      • Tourist attraction-Nyasa dc Video
    • speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Progress project

BARAZA la Madiwani latoa motisha kwa watumishi

Posted on: June 19th, 2025

Na Byarugaba Innocent, Nyasa DC

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mhe. Stewart Nombo ameongoza kikao cha mwisho cha baraza Maalum la mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG) lililoketi kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri Jumatano tarehe 18 Juni, 2025 kwa ajili ya kupitia na kujadili hesabu za serikali kwa Mwaka wa fedha 2023/2024 za Halmashauri ya Nyasa.

Mkaguzi Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma Nicholaus Killinga ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwa kuendelea kupata hati safi baada ya kupitia taarifa ya ukaguzi wa hesabu za Mwaka 2023/2024.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Stewart Nombo amesema mafanikio yaliyofikiwa katika halmashauri ya Nyasa yanatokana na kufanyakazi kwa mshikamano na ushirikiano baina ya Chama Cha Mapinduzi, Wahe. madiwani na wataalam kwani mara zote wameendelea kuongea lugha moja wanapokuwa kwenye agenda za mapato na matumizi.

Kwa upande wake katibu tawala wa Mkoa wa Ruvuma Mary Makondo aliyefika kwa niaba ya Mkuu Mkoa wa Ruvuma amewapongeza Wahe. madiwani kwa kuisimamia vema halmashauri, Mkurugenzi na wataalam wake kwa kuendelea kufanyakazi kwa ushirikiano, weledi na ubunifu na kufanikisha kupata hati safi na kwamba hayo ndio malengo ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwahudumia wananchi

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Khalid Khalif kando ya kupokea pongezi kwa niaba ya wataalam na kuwashukuru Wahe. madiwani kwa ushirikiano walioonyesha katika kipindi chao cha uongozi, alieleza kuwa wapo watumishi wawili Ratifa Mchomvu na CPA Albert Mtungi kutoka kitengo cha fedha na uhasibu waliokuwa chachu ya mafanikio hayo kwa kufunga hesabu za Halmashauri kitaalam  na kuwaomba Baraza la Madiwani kuutambua Mchango wao kwa kuwapa tuzo maalum kama sehemu ya Motisha.

Aidha, Mkurugenzi Khalid alieleza zawadi zinazotolewa  kwa watumishi hao ni cheti cha pongezi na fedha taslimu kiasi cha shilingi 200,000.00 kwa kila mmoja ikiwa ni sehemu ya halmashauri kuutambua mchango wao na kutoa hamasa kwa watumishi wengine kufanya kazi kwa kujituma zaidi na kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo.

CPA Albert Mtungi akiongea kwa niaba ya wanufaikaji amelishukuru baraza la madiwani kwa kuutambua mchango wao na kwamba kitendo cha kuwapa zawadi kimewapa nguvu zaidi ya kufanyakazi kwa ubunifu na weledi huku sheria kanuni, taratibu, miongozo ya fedha iliyopo ikizingatiwa kwa maslahi mapana ya Halmashauri ya Nyasa na Taifa kwa ujumla.

 

Announcements

  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya wilaya ya Nyasa December 01, 2025
  • TANGAZO LA KUHAKIKI UMILIKI WA ARDHI NYASA August 30, 2021
  • MAREKEBISHO YA TAREHE YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 17, 2022
  • TANGAZO la nafasi ya kazi February 03, 2023
  • View All

Latest News

  • Balozi wa Tanzania nchini Malawi atembelea Wilaya ya Nyasa

    December 06, 2025
  • Maonesho ya Nane Nane Kanda za Nyanda za juu kusini , Mguu sawa Kuanza leo

    August 01, 2025
  • UTEKELEZAJI KAMPENI YA CHANJO YA MIFUGO YAANZA NYASA

    July 12, 2025
  • MAKUNDI SOGOZI YA WHATSAAP YAPASWA KUJADILI MAENDELEO

    July 12, 2025
  • View All

Video

TUNAMPONGEZA Rais Samia kwa kutuletea maendeleo Nyasa na kumteua Dkt Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza
More Videos

Quick Links

  • Ruvuma Regional Website
  • Songea Municipal Website
  • Songea District Website
  • Mbinga Town Website
  • Mbinga District Website
  • Madaba District Website
  • Tunduru District Website
  • EGA WEBSITE
  • Namtumbo District Website

Related Links

  • National website
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistic

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Nyasa District Council

    Postal Address: Box 90 Mbamba bay

    Telephone: 025 -2952003

    Mobile:

    Email: ps.ded@nyasadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Nyasa District Council. All rights reserved.